Posts

Showing posts from August, 2020

TRA YAZINDUA MFUMO WA KUWASILISHA RITANI KIELEKTRONIKI

Image
  Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dkt. Edwin P. Mhede (mwenye tai nyekundu) akiongea na Wajumbe wa Bodi, Menejimenti ya TRA pamoja na Waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Mfumo wa Kuwasilisha ritani za Kodi (e-filing) leo Jijini Arusha. Mkurugenzi wa Mifumo ya TEHAMA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) (kushoto) akielezea namna Mfumo wa Kuwasilisha Ritani za Kodi unavyofanya kazi mbele ya Wajumbe wa Bodi, Menejimenti ya TRA pamoja na Waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Mfumo wa Kuwasilisha ritani za Kodi (e-filing) leo Jijini Arusha. Wajumbe wa Bodi, Menejimenti ya TRA pamoja na Waandishi wa habari wakifuatilia uzinduzi wa Mfumo wa Kuwasilisha ritani za Kodi (e-filing) leo Jijini Arusha. ……………………………………………………………….. Na Rachel Mkundai, Arusha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeanzisha mfumo wa uwasilishaji wa ritani za kodi kwa njia ya kielektroniki (e-Filing System) ukiwa na lengo kurahisisha uwasilishaji wa ritani za kodi na kupunguza gharama kwa upand...

NANENANE DODOMA KUANZISHA MAONESHO YA KIMATAIFA YA UTALII WA MIFUGO

Image
  Mwakilishi wa Wakuu wa Mikoa ya Singida na Dodoma  kwenye  Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati, ambaye  pia ni  Mkuu ya Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi  Athuman Mukunda akijaribu  kuendesha Trekta kwenye maonesho hayo  leo, aliye pembeni yake ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Elisante Ole Gabriel,  walio chini  mwenye miwani ni Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Anjelina Lutambi na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Injinia Jackson Masaka wakishuhudia tukio hilo. Picha na John Mapepele Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Anjelina Lutambi akitoa salamu za Mkoa wa Singida kwenye Paredi Maalum la Mifugo. Picha na John Mapepele   Mfugaji wa Mifugo Juma Seleman kutoka  Mpwapwa akipitisha Ng’ombe wake  Mashindano maalum ya Paredi ya mifugo iliyofanyika kwenye maonesho ya nanenane kanda ya kati kwenye viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma. Picha na John Mapepele Viongozi...