Posts

Showing posts from November, 2022

BARAZA LA WAFANYAKAZI LATAKIWA KISIMAMIA UTENDAJI KAZI, NIDHAMU

Image
 Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Bw. Godfrey Nyaisa, amewataka wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi kuhakikisha kuwa wanasimamia ipasavyo  utendaji kazi pamoja na nidhamu ya watumishi ili kuongeza ufanisi wa Taasisi. Bw. Nyaisa ametoa agizo hilo leo tarehe 11 Novemba, 2022 wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza  la Wafanyakazi  kinachofanyika mkoani Morogoro. Bw. Nyaisa amesema kwakuwa Baraza la Wafanyakazi ni chombo cha ushirikishaji wa watumishi na linaundwa na wajumbe kutoka Menejimenti ya BRELA, viongozi wa Chama cha Wafanyakazi (TUGHE)  na wawakilishi wa watumishi kutoka idara mbalimbali, wajumbe wote wanao wajibu wa kusimamia utendaji kazi pamoja na nidhamu ya watumishi ili kutoharibu taswira ya Taasisi. Bw. Nyaisa amesema pia  viongozi wa  TUGHE kama wajumbe wa Baraza wanapaswa kufuatilia maslahi ya wafanyakazi kwa kushirikiana na Menejimenti, hivyo  wanapoona  ...

Mhe. Mhengerwa -Tamasha la Sanaa Bagamoyo ni la kimataifa, Makamu wa Rais afafanua kuwa Sanaa inaongoza katika ukuaji wa uchumi nchini

Image
  Na John Mapepele Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema  Serikali imefanya  maboresho makubwa   kwenye Tamasha la mwaka huu la 41 la Utamaduni na Sanaa   Bagamoyo kuwa la kimataifa ambapo limeshirikisha nchi mbalimbali duniani ili kuitangaza Tanzania na utamaduni wake duniani. Kauli hiyo ameitoa leo wakati akimkaribisha Makamu wa Rais Mhe, Dkt. Philipo Mpango kuzindua rasmi tamasha hili kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano. Mhe. Samia  Suluhu Hassan. Ameongeza kuwa tamasha hili limeshirikisha vikundi vya wasanii kutoa mataifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Canada, Zambia, Burundi na Visiwa vya Mayote kutoka nchini Ufaransa. “Mwaka huu tumeendelea  kuliboresha Zaidi tamasha hili kutoka kuwa tamasha la mazoea la wanafunzi wa sanaa hapa chuoni ili kulipatia hadhi zaidi ya kuwa tamasha la kimataifa.” Amesisitiza Mhe. Mchengerwa Aidha amesema wameteleza maelekezo ya Mhe. Rais ya kutaka kuendeleza tamasha hili n...

Mhe. Kikwete aipongeza Wizara kwa kukuza Sekta ya Sanaa kwa kasi, adai ina mchango mkubwa kwenye uchumi

Image
  Na John Mapepele Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ameipongeza   Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo  kwa  kazi kubwa inayoifanya   ambayo imesababisha kuwa miongoni mwa sekta zinazokuwa kwa kasi na kuchangia kwa kiasi kikubwa kwenye uchumi wa Taifa kwa ujumla. Mhe. Kikwete ameyasema haya Usiku wa kuamkia leo Novemba 6, 2022 akiwa Mgeni wa rasmi kwenye uzinduzi wa albamu ya Ommy Dimpoz iitwayo Dedication mara baada ya kukaribishwa kutoa hotuba yake na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye amekuwa mgeni wa heshima kwenye uzinduzi huo. Amefafanua kuwa katika awamu hii ya Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan tasnina ya muziki wa kizazi kipya imekua kwa kasi na kupata mafanikio makubwa ukilinganisha awamu zilizopita.    “Kila siku nikiangalia kwenye televisheni naona wanamuziki na wasanii wapya hali a...