Posts

Showing posts from December, 2022

RAIS SAMIA MGENI RASMI KATIKA ZOEZI LA UFUNGUZI BWAWA LA MWALIMU NYERERE DESEMBA 22,2022

Image
  Waziri wa Nishati Januari Makamba(wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la kuanza kujaza maji katika bwawa la Julius Nyerere(JNHPP) lililopo Rufiji mkoani Pwani.Tukio hilo la kuanza kujaza maji linatarajiwa kufanyika Desemba 22 mwaka huu ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.Kulia kwenye picha hiyo ni Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO Maharage Chande na kushoto ni viongozi kutoka Wizara ya Nishati. Baadhi ya wakandarasi wa ujenzi wa Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere wakiwa kwenye kikao cha Waziri wa Nishati Januari Makamba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuanza kujazwa maji kwa bwawa hilo tukio ambalo litafanyika Desemba 22 mwaka huu. Muonekano wa handaki la kuchepusha maji kama ambavyo linaonekana baada ya ujenzi wake kufikia asilimia 78.68. Waziri wa Nishati Januari Makamba akijadiliana jambo na maofisa wa TANESCO pamoja na Wizara ya Nishati leo Desemba 18 mwaka 2022 baada ya...

BENKI YA CRDB, VISA KULETA MAPINDUZI SEKTA YA UTALII NA USAFIRISHAJI KUPITIA KADI ZA KIDIJITALI

Image
  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) akifanya mazungumzo na Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Visa International, Alfred Kelly kuhusu ushirikiano baina ya taasisi hizo katika kuanzisha huduma za malipo ya kidijitali katika sekta ya utalii. Mkutano huo ulifanyika wakati wa Mkutano wa Viongozi wa Marekani na Afrika Washington DC Marekani siku ya Ijumaa tarehe 16 Desemba 2022. Washington DC 16 Desemba 2022 - Benki ya CRDB Plc, Benki inayoongoza kwa uvumbuzi wa kidijitali nchini, na kampuni ya kimataifa ya mifumo ya malipo ya Visa International, leo wamekubaliana kuhusu ushirikiano wa kuanzisha huduma ya kadi za kidijitali kwa ajili ya kuboresha huduma za malipo katika sekta ya utalii nchini. Kupitia kadi hizo, Benki ya CRDB na Visa wanatarajia kutoa njia rahisi zaidi ya kufanya na kupokea malipo kwa wateja na makampuni ya sekta ya utalii na usafirishaji kwa usalama na uharaka kulinganisha na mifumo mingine ya malipo. Ushirikiano huo mpya na Visa, kwa...

JAFO AZINDUA JOSHO SIMANJIRO

Image
  Waziri Jafo azindua josho Simanjiro kupitia Mradi wa EBARR Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amezindua josho la kuogeshea mifugo katika Kijiji cha Irkujit wilayani Simanjiro mkoani Manyara ambalo limejengwa kupitia Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR). Akizungumza na wananchi wakati wa ziara ya kukagua mradi huo Desemba 15, 2022 amewapongeza wananchi hao kwa kuibua mradi huo ambao unawawezesha kuikinga mifugo yao kwa magonjwa yaenezwayo na kupe na mbung’o. Dkt. Jafo amesema josho hilo linalotarajiwa kuhudumia wananchi takriban 30,000 wa kijiji hicho na vijiji jirani ni matunda ya Serikali katika kuhakikisha inawasidia wananchi kupambana na athari za mabadiliko ya Tabianchi. Alisema athari za mabadiliko ya tabianchi ni kubwa zinazosababisha maeneo ya nchi kuwa na ukame ambao ni chanzo cha kukosekana kwa mvua, hivyo matokeo yake ni kukauka kwa vyanzo vya maji vikiwemo mabwawa. “Nd...

MENEJIMENTI YA TAWA YATAKIWA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO

Image
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb)ameitaka  menejimenti  Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ifanye kazi kwa ushirikiano ili kuiwezesha taasisi hiyo kutimiza malengo yaliyowekwa.  Mhe. Mary Masanja ametoa kauli hiyo leo jijini Mwanza mara baada ya kuitembelea menejimenti ya TAWA inayoendelea na mafunzo ya uongozi  katika Chuo cha Usimamizi wa  Wanyamapori Pasiansi. Amewaeleza kuwa utendaji kazi wenye kuzingatia  ushirikiano na Upendo ni nguzo muhimu itakayowawezesha  kurekebishana na kukosoana kiutendaji  kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa. Aidha, amesisitiza kuwa ni vyema menejimenti hiyo ikajiwekea utaratibu wa kujadili changamoto mbalimbali pamoja ili iweze  kufika mbali kiutendaji. "Mwenzako anapokutana na changamoto yoyote ichukulie kama ni yako. Tunahitaji  tufanikiwe kwa kutatua changamoto zinazotukabili kwa pamoja " amesisitiza Mhe. Masanja. Mafunzo hayo yenye len...

RAIS DKT. SAMIA, WAZIRI MCHENGERWA WATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA NA SHUKRAN TUZO ZA FILAMU 2022

Image
  Na John Mapepele Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa wametunukiwa Tuzo maalum ya shukrani kwa mchango wao katika kuleta mapinduzi makubwa kwenye sekta ya Sanaa. Tuzo hizo zimetolewa kwenye kilele cha utoaji wa Tuzo za Filamu 2022 uliofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye kituo cha Kimataifa cha Mkutano Arusha, AICC. Awali kabla ya kukabidhi Tuzo hizo, Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Filamu, Dkt. Kiagho Kilonzo amesema Mhe. Mchengerwa amechaguliwa kwa kuzingatia mchango wake mkubwa alioufanya katika kipindi kifupi tangu achaguliwe kusimamia sekta hiyo ambayo inaongoza kwenye kuchangia ukuaji wa uchumi. Amesema maelekezo ambayo amekuwa akiyatoa na kuyasimamia yamesaidia kukuza Sekta hiyo kwa kiwango kikubwa. "Ni kutokana na maelekezo thabiti ya Mheshimiwa Waziri ndiyo maana leo tunashuhudia kufanyika kwa mafanikio makubwa utoaji wa Tuzo wa msimu wa pili" amefafanua Kilonzo Tuzo ya Mhe. Rais ilikabidhi...

Mhe. Mchengerwa ahimiza kumuenzi Bibi Titi

Image
  Na John Mapepele Waziri Wa Utamaduni, Sanaa, Mhe. Mohamed Mchengerwa amehimiza umuhimu wa kumuenzi mwanaharakati  mwanamke, Bibi Titi Mohamed aliyefanya kazi kwa karibuni na Mwalimu Julisu Nyerere katika harakati za kuleta uhuru wa Tanganyika. Akizungumzia tamasha  la Bibi Titi Mohamed litakalofanyika  wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani, Mhe. Mchengerwa kwenye kipindi cha 360 cha kituo cha televisheni cha Clouds leo ambapo amesema  Bibi Titi ni alama ya mabadiliko katika suala zima la ushiriki wa wanakwake katika harakati hizo na kuleta mabadiliko.  “Ukimzungumzia Bibi Titi Mohamed unazungumzia alama ya mabadiliko, unazungumia alama ya kutoka kutoamini kuja katika kuamini kwa sababu Bibi Titi  mwenyewe aliamini kwamba tunaweza kujikomboa,” amesema. Amesema ni vigumu kuzungumzia mabadiliko ya kisiasa ya kuwaingiza wanawake katika siasa, ushawishi wa katika siasa, uchumi, matumizi ya Kiswahili,  bila kumzungumzia Bibi Titi Mohamed.   Amesema...